Mgomo wa walimu .

Kwa muda mrefu sasa Serikali imekuwa kwenye mgogoro wa kimaslahi na walimu, jambo lililofanya Chama cha Walimu nchini (CWT) kuwahamasisha wanachama wake kuingia kwenye mgomo usio na kikomo. Mara zote ambazo CWT ilipanga kuanza mgomo, azma yao ilikatishwa na amri ya Mahakama ama mazungumzo baina ya chama hicho na serikali. Vitu ambavyo walimu wamekuwa wakidai ni pamoja na kulipwa malimbikizo ya fedha za likizo, kupandiswa madaraja na kutaka mishahara yao iongezwe. Madai hayo hayatofautiani na yale ya walimu wa Kenya ambao wamekuwa kwenye mgomo kwa majuma mawili licha ya kuwapo kwa amri ya mahakama iliyowataka kurudi darasani.

Comments